Shairi: Dunia Bahari Kuu

Dunia duara, ndivyo asemavyo babu

Katu mie sipingi,anazo sababu

Kwani ina vituko,tena vingi ajabu

Dunia bahari,mja sipige mbizi

Kingo zilizofungaka,mwisho haunekani

Inazo sifa tajika,nzuri na za huzuni

Mara moja tacheka,ghafla ije huzuni

Dunia bahari,mja sipige mbizi

Ina meno makali,zaidi ya msumeno

Yanakata vikali,usibaki hata mkono

Wewe mwenye akili,jiepushe usiwe mfano

Dunia bahari,mja sipige mbizi

Dunia ina madhila,sishindane nayo

Ina chache fadhila,epukana nayo

Siifanyie hila,takutia jongomeo

Dunia bahari,mja sipige mbizi

Ina makali mawimbi,usije ukasombwa

Dunia ni hatari,haitambui mpendwa

Inavyo vingi vitimbi,chunga usije naswa

Dunia bahari, mja sipige mbizi

Dunia gae bovu,lisilo thamani

Imejaa mauvu,haina tena amani

Chunga usiipe shavu,haina shukrani

Dunia bahari,mja sipige mbizi

Kaditama nafika,yanipasa kuondoka

Nasaha hiyo shika,isije tena ponyoka

Usije danganyika,mabaya yakakufika

Dunia bahari,mja sipige mbizi

@Malenga wa bara

*Ayieko Jakoyo*

Ayieko Jakoyo ni mwandishi wa mashairi na makala mengine katika lugha ya kiswahili na kiingereza

Ayieko jakoyo

Ayieko jakoyo

Ayieko Jakoyo is a seasoned writer and a poet in both English and Kiswahili(Ushairi). Having learnt in a rural or rather village primary and secondary school, I took my time to interact with various people in the society based on age and gender. My writing has been shaped by the daily occurances in the typical African society My literary star was lit and brightened by the famous poet Robert Frost. I loved his wordplay and how he addressed concrete issues through poetry. I always lived to write and sell out as he did in his time. I deeply got into writing when my article "Girl child's plea" did well in the 2009 National music festival for secondary schools. When I joined The university of Eldoret, I joined the C. O. F. F. E. E which is an association for the lovers of art and the BRIDGE campus magazine. Since then my poetry is doing well on various platforms. I have also joined jubilant stewards of Africa and I am looking forward to give my readers the best. Check my wordpress, sebbyjakoyo.wordpress.com for more articles. Find me on Fb as Ayieko Jakoyo And twitter as Jakoyo_jnr

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *